WOSIA


X.

AGIZO LA KUMI

UAMINIFU KATIKA KUTIMIZA KANUNI TAKATIFU

 

"Anayeishi katika kanuni anaishi na Mungu". „Kanuni" maana yake ni Katiba na Desturi zetu ambazo zinatueleza tafsiri ya kiroho ya Kanuni takatifu. Kuwa mwaminifu katika Kanuni ni njia ya kweli na ya uhakika katika kuufikia utakatifu. Hatuwezi kufikiri njia bora zaidi.

Kanuni zetu ni hazina yetu kwa sababu kwetu sisi ni onesho la wazi na la uhakika la mapenzi ya Mungu kwetu sisi na ndio maana zinapaswa kuwa kwetu na thamani isiyo na mwisho. Hatuhitaji kuchoka katika kuzitafuta, sisi tunazo na tunaishi ndani yake, zimetuzunguka katika kila hatua. Kama ndege angani na samaki majini, hivi na sisi tumezamishwa katika mapenzi ya Mungu, yaonyeshwayo katika Kanuni zetu takatifu. Ina maana gani kusema kuunganika na Mungu? Ina maana kuunganika na mapenzi yake. Ni nani ambaye kwa undani ameunganika kabisa na Mungu? Yule ambaye katika kila hatua anayatimiza mapenzi ya Mungu na mapenzi yake ameyaunganisha kabisa na ya Mungu. Kwa uhakika Kanuni zetu takatifu zinatuongoza katika kuunganika na mapenzi ya Mungu, kwa sababu zinatuonesha ni wapi penye mapenzi ya Mungu na zinatuwezesha kuyatimiza kila wakati.

Tuzipende, tuzipende kwa moyo wetu wote Kanuni zetu takatifu, tujitahidi kuzifuata kwa uaminifu mkubwa. Tuziingize ndani ya mioyo yetu na tuzitafakari. Zenyewe ndio nguvu zetu, furaha yetu, alama inayotuongoza njia ya mbinguni, mwanga wetu, maana zinaeleza wazi mapenzi ya Mungu.

Tusijiondoe katika ukamilifu mwaminifu wa Kanuni takatifu. Zenyewe zatuonya wakati mwingine, zinazuia tabia 32

yetu mbaya ya asili, na hiyo ni nzuri hata kama tabia haipendi. Kanuni zinatusaidia kuondoka kwenye vifungo vya u "mimi" duniani na kutuinua juu, kuelekea kwa Mungu, kwa mbawa za mapenzi yake.

Basi tuchukue juu yetu kwa ushujaa na kwa uzuri mzigo wa Kanuni takatifu. Huu mzigo kwa anayempenda Mungu, ni mwepesi na mtamu, kwa sababu ni mapenzi ya Mungu, mema yasiyo na mwisho, matakatifu na yenye hekima: ni hazina yetu, ni yote yetu duniani.